SHERIA Published on December 4, 2025
Waliojihusisha na ukiukwaji wa sheria kwa kujiingiza kwenye biashara haramu ya madawa ya kulevya, mali zao zataifishwa.
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imetaifisha mali zenye thamani ya shilingi bilioni 3.304 zinazodaiwa kupatikana kupitia biashara haramu ya dawa za kulevya.
Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi endelevu za kudhibiti uhalifu wa dawa za kulevya, ambapo mamlaka hiyo pia imefanikiwa kukamata zaidi ya kilo 3,799 za dawa za kulevya, kuteketeza ekari 18 za mashamba ya bangi na kuwakamata watuhumiwa 84.
No Video Available